Prof Raphael Chibunda Awataka Wanafunzi Wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo Kampasi Ya Mizengo Pinda Kutumia Vyema Elimu Wanayoipata Ili Kukabiliana Na Changamoto Ya Ajira

Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Prof. Raphael Chibunda, amewataka wanafunzi wa Kampasi ya Mizengo Pinda kutumia vyema Elimu wanayoipata ili waweze kukabiliana na changamoto ya ajira kwa kujiunga na kujisajili  katika vikundi ili waweze kupata pesa na kuendesha miradi ya ujasiriamali kama ufugaji wa nyuki, kutoa elimu kwa jamii juu ya ufugaji bora na wenye tija ili kujiongezea kipato na kuachana na dhana ya kusubiria ajira kutoka Serikalini.

Prof. Chibunda ameyasema hayo   tarehe 7 /11/2022, alipotembelea Kampasi ya Mizengo Pinda na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kujionea maeneo ya mradi wa upanuzi wa kampasi hiyo.

Pia Prof Chibunda ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Mh. Samia Suluhu Hassan, kwa kutenga kiasi cha shilingi Bilioni ishirini kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika Kampasi hiyo.

Wakati huo huo Prof. Chibunda alipata nafasi ya kutembelea eneo linalochimbwa kisima cha maji katika Kampasi hiyo na kuendelea kumshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania M.h Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa pesa za maendeleo katika chuo chetu.

Pia, makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof Chibunda akipokea taarifa kutoka kwa katibu wa  kamati ya ufuatiliaji wa ardhi kwa ajili ya upanuzi wa Kampasi ya Mizengo Pinda.

 

Related Posts

DC MONGERA APONGEZA UBUNIFU WA SUA KAMPASI YA MIZENGO PINDA MAADHIMISHO YA WIKI YA NYUKI TABORA

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Mheshimiwa Gerald Mongera, amekipongeza Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mizengo Pinda,...

SUA KAMPASI YA MIZENGO PINDA YAZITIKISA SHULE ZA SEKONDARI MLELE: YAHAMASISHA TAALUMA NA KUTANGAZA FURSA ZA UDAHILI

Katika juhudi za kuendeleza hamasa ya kielimu na kusogeza huduma za elimu ya juu karibu na jamii, Chuo Kikuu cha...

SUA Kampasi ya Mizengo Pinda Yachochea Ndoto za Wanafunzi Halmashauri ya Mpimbwe kupitia Ziara ya Hamasa.

Katika jitihada za kusogeza elimu ya juu karibu na jamii na kuibua hamasa ya kimasomo, Chuo Kikuu cha Sokoine cha...