Bodi ya Ukaguzi ya SUA Yafanya Ziara katika Kampasi ya Mizengo Pinda

Katika jitihada za kuimarisha ubora wa elimu na utafiti, Bodi ya Ukaguzi ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo (SUA) ilifanya ziara ya kikazi kwenye Kampasi ya Mizengo Pinda tarehe 13 Machi 2024. Ziara hii ilikuwa na lengo la kukagua maendeleo na shughuli mbalimbali zinazoendelea kampasini, ikiwa ni pamoja na miradi mipya ya maendeleo. Wajumbe Waliotembelea, Dkt. Charles Lyimo (Mwenyekiti),Arnold Mbwambo (Katibu Msaidizi),Tryphone Ngoja na Dismas Myinga.

Wajumbe walipokelewa kwa mikono miwili na timu ya Idara ya Manunuzi, wakiongozwa na Bwana Daudi Ally Fungo. Walipata fursa ya kutembele maeneo muhimu ya kampasi, ikiwemo kiwanda cha matofari, mashine ya kuchakatia asali, na chumba cha kompyuta kinachotumiwa na wanafunzi kwa ajili ya kujifunzia kwa vitendo.

Ziara hii ilileta mwanga mpya kuhusu maendeleo ya kampasi, hasa katika kuendeleza elimu na uchumi wa kampasi. Vifaa vipya vilivyonunuliwa vinaashiria hatua kubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. Kituo cha kutolea huduma za afya kilichokaguliwa kinaonesha dhamira ya SUA katika kuhakikisha afya bora kwa wanafunzi na wafanyakazi.

Kampasi ya Mizengo Pinda, ikiwa ni sehemu ya SUA, inaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kukuza elimu na kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya jamii. Bodi ya Ukaguzi imejionea na kuridhika na maendeleo yaliyopo, na ina imani kuwa kampasi itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa.

Related Posts

DC MONGERA APONGEZA UBUNIFU WA SUA KAMPASI YA MIZENGO PINDA MAADHIMISHO YA WIKI YA NYUKI TABORA

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Mheshimiwa Gerald Mongera, amekipongeza Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mizengo Pinda,...

SUA KAMPASI YA MIZENGO PINDA YAZITIKISA SHULE ZA SEKONDARI MLELE: YAHAMASISHA TAALUMA NA KUTANGAZA FURSA ZA UDAHILI

Katika juhudi za kuendeleza hamasa ya kielimu na kusogeza huduma za elimu ya juu karibu na jamii, Chuo Kikuu cha...

SUA Kampasi ya Mizengo Pinda Yachochea Ndoto za Wanafunzi Halmashauri ya Mpimbwe kupitia Ziara ya Hamasa.

Katika jitihada za kusogeza elimu ya juu karibu na jamii na kuibua hamasa ya kimasomo, Chuo Kikuu cha Sokoine cha...