Mkuu wa mkoa wa katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko atembelea banda la chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda katika maonesho ya nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya John Mwakangale Mkoani Mbeya

Katika banda hilo, Mkuu wa Mkoa wa Katavi alipata nafasi ya kuona na kupata maelezo juu ya  bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Chuo ikiwemo mafuta ya alizeti na asali na mara baada ya kupatiwa maelezo juu ya bidhaa hizo, Mhe. Mrindoko alizawadiwa mafuta ya alizeti.

Mhe. Mwanamvua Mrindoko akipokea zawadi ya mafuta ya alizeti kutoka Kwa mhadhiri msaidizi wa Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda ndugu Evaristus Magani

Mhe. Mwanamvua Mrindoko aliambatana na mwenyeji wake Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Mhe. Rodrick Mpogolo ambaye naye alikabidhiwa zawadi ya asali inayozalishwa na Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda.

Mhe. Rodrick Mpogolo akipokea zawadi ya asali kutoka Kwa Afisa udahili wa Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda ndugu Abel Magembe Lugimba

Wananchi nao wanaendelea kujitokeza kujifunza na kujionea bidhaa mbalimbali zitokanazo na rasilimali nyuki na kilimo katika maonesho hayo ambayo kilele chake ni tarehe 08- 08- 2023.

Wananchi mbalimbali wakiendelea kujifunza na kujionea bidhaa mbalimbali zitokanazo na rasilimali nyuki na kilimo katika banda la chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda

Related Posts

DC MONGERA APONGEZA UBUNIFU WA SUA KAMPASI YA MIZENGO PINDA MAADHIMISHO YA WIKI YA NYUKI TABORA

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Mheshimiwa Gerald Mongera, amekipongeza Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mizengo Pinda,...

SUA KAMPASI YA MIZENGO PINDA YAZITIKISA SHULE ZA SEKONDARI MLELE: YAHAMASISHA TAALUMA NA KUTANGAZA FURSA ZA UDAHILI

Katika juhudi za kuendeleza hamasa ya kielimu na kusogeza huduma za elimu ya juu karibu na jamii, Chuo Kikuu cha...

SUA Kampasi ya Mizengo Pinda Yachochea Ndoto za Wanafunzi Halmashauri ya Mpimbwe kupitia Ziara ya Hamasa.

Katika jitihada za kusogeza elimu ya juu karibu na jamii na kuibua hamasa ya kimasomo, Chuo Kikuu cha Sokoine cha...