Makamu Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo Prof Raphael Chibunda Awataka Watumishi Wa Kampasi Ya Mizengo Pinda Kufanya Kazi Kwa Ushirikiano

Prof. Chibunda amewataka watumishi wa Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda kufanyakazi kwa ushirikiano ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kampasi hiyo. Aliyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi ya siku mbili katika Kampasi ya Mizengo Pinda Novemba 7 – 8, 2022.

Katika ziara hiyo, Prof. Chibunda alipokea ripoti ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Kampasi hiyo na kupata fursa ya kutembelea miradi hiyo.

Pia, Prof. Chibunda aliongeza kusema kwamba kupitia serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuboresha sekta ya elimu ya juu nchini ikiwemo Kampasi ya Mizengo Pinda.  Kiasi cha pesa takribani bilioni ishirini zimetengwa kwa ajili ya kuboresha na kuendeleza Kampasi ya Mizengo Pinda. Pesa hizo zinatarajiwa kutumika kujenga majengo matatu ambayo ni jengo la Taaluma linalokadiriwa kuchukua wanafunzi zaidi ya elfu mbili (2000) kwa wakati mmoja, maabara za kufundishia pamoja na dahalia.

Related Posts

Mafunzo Elekezi kwa Wafanyakazi wa Kampasi ya Mizengo Pinda kuhusu Ujazaji wa Mfumo wa Taarifa za Utendaji Kazi na Usimamizi wa Wafanyakazi wa Umma (PEPMIS).

Mafunzo ya kipekee yaliyofanyika katika Kampasi ya Mizengo Pinda yameleta mwanga mpya kwa wafanyakazi. Mafunzo hayo, yaliyoandaliwa na Ofisi ya...

Chairperson Professor Josiah Katani Conducts a Special Academic Committee Meeting at Mizengo Pinda Campus.

The Principal, Prof. Josiah Katani plays a pivotal role in overseeing the proceedings and ensuring that the committee’s recommendations align...

Bodi ya Ukaguzi ya SUA Yafanya Ziara katika Kampasi ya Mizengo Pinda

Katika jitihada za kuimarisha ubora wa elimu na utafiti, Bodi ya Ukaguzi ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo (SUA)...