Safari ya Mhitimu wa SUA Kuelekea Ujasiriamali wa Bidhaa Zitokanazo na Rasilimali  Nyuki

Katika picha, aliyeshika chupa za asali ni Dwasi Denis Johnson, mhitimu wa Shahada ya Sayansi ya Awali ya Usimamizi wa Rasilimali Nyuki. Anatumia ujasiriamali wa bidhaa zitokanazo na rasilimali nyuki, kama asali ya nyuki wakubwa na wadogo, katika maonesho ya Wiki ya Mwanakatavi ambayo hufanyika kila mwaka mkoani Katavi. Maonesho haya yana lengo la kuwakutanisha wajasiriamali, taasisi, wakulima, wafugaji na kutangaza utalii na fursa zote zipatikanazo katika mkoa wa Katavi.

Bw. Dwasi amemshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpimbwe, Bi. Shamimu Mwariko, kwa kuendelea kuwapa ushirikiano kama wajasiriamali wa Halmashauri ya Mpimbwe.

Kwa sasa, Bw. Dwasi ana mizinga ishirini (20) iliyopo kwenye kijiji cha Kanindi, yenye uwezo wa kutoa lita 15 hadi 20 za asali. Hivyo, Bw. Dwasi anawaomba wadau ambao wanaweza kumsaidia kupata mizinga ya kisasa inayogharimu kiasi cha shilingi milioni mbili (2,000,000) ili aweze kuzalisha zaidi asali.

Katika picha: Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Rungwa wakipata elimu kuhusu uzalishaji wa asali kupitia mdudu nyuki na kalenda sahihi ya uandaaji wa mizinga. Elimu hii ilitolewa walipotembelea banda la Halmashauri ya Mpimbwe katika Maonesho ya Wiki ya Mwanakatavi.

Related Posts

Mwenyekiti wa Bodi, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mizengo Pinda, Dkt. Zacharia Malley aongoza shughuli ya upandaji miti SUA Kampasi ya Mizengo Pinda

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mizengo Pinda, Dkt. Zacharia Malley, ameongoza shughuli...

Final Year Bee Resources Management Students of SUA Mizengo Pinda Campus Defend Special Projects

On February 19, 2026, thirty-eight final year students pursuing a Bachelor of Science in Bee Resources Management at the Mizengo...

Prof. Anna Sikira Urges First-Year Students at Mizengo Pinda Campus to Become Ethical Leaders and Responsible Citizens

Mizengo Pinda Campus, Sokoine University of Agriculture—21 November 2025 Sokoine University of Agriculture (SUA), Mizengo Pinda Campus, has concluded a...