Siku ya Wanawake Duniani: Kusherehekea Mafanikio ya Wanawake na Kuhamasisha Umoja Katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)

Profesa Josiah Katani         (Rasi wa Ndaki)

Rasi wa Kampasi ya Mizengo Pinda, Profesa Josiah Katani, Awapongeza Wanawake Katika Siku ya Wanawake Duniani.

Dunia inaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani tarehe 8 Machi kila mwaka. Siku hii ni muhimu kwa kutambua mchango wa wanawake katika jamii na kuhamasisha usawa wa kijinsia. Rasi wa Kampasi ya Mizengo Pinda, Profesa Josiah Katani, ameungana na jamii ya kimataifa kuwapongeza wanawake wote nchini na duniani kote kwa mafanikio yao katika nyanja mbalimbali

 

Wanawake wa SUA Katika Uongozi, Elimu, na Maendeleo ya Kiuchumi

Profesa Anna Sikira (Naibu Rasi wa Ndaki-                Taaluma)

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kinajivunia kuwa na wanawake wenye uwezo na ushawishi mkubwa katika uongozi, elimu, na maendeleo ya kiuchumi. Baadhi ya mifano ni pamoja na:

Profesa Anna Sikira, Naibu Rasi wa Ndaki Taaluma, Utafiti, na Ustawi wa Kitaaluma:Profesa Sikira anaongoza juhudi za kuimarisha taaluma na utafiti katika chuo kikuu. Mchango wake unathibitisha uwezo wa wanawake katika nafasi za uongozi wa kitaaluma.

 

Ms. Rachel Mshana
(Mshauri wa Wanafunzi)

Ms. Rachael Mshana, Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Wanafunzi: Mshana anahakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza na kufanikiwa, na kuchangia katika ustawi wa jamii.

Ms. Debora Magesa
(Mkuu wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano)

Ms. Debora Magesa, Mkuu wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano: Magesa anaimarisha mifumo ya TEHAMA katika kampasi, na kuhakikisha ufanisi wa mawasiliano na ufikiaji wa habari. 

Wito kwa Wanawake Kuendelea Kujiendeleza na Kuchukua Nafasi za Uongozi

Profesa Katani anawahimiza wanawake kuendelea kujiendeleza kielimu, kufanya kazi kwa bidii, na kujituma katika majukumu yao. Anawasisitiza  kujiamini na kuthubutu kuchukua nafasi za uongozi. Wanaume pia wanahimizwa kuunga mkono juhudi za wanawake na kushirikiana nao katika kujenga jamii yenye usawa na maendeleo endelevu.

Kumbukumbu kwa Vijana wa Kiume Katika Siku Hii

Wakati tunaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, ni muhimu kuwakumbusha vijana wa kiume wajibu wao katika kuleta maendeleo. Wanapaswa kushirikiana na wanawake katika kupambana na ubaguzi wa kijinsia na kujenga jamii bora kwa wote.

Mwisho, Profesa Katani anampongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuimarisha maisha ya wanawake na vijana kupitia miradi kama vile Kujenga Kesho Iliyo Bora (BBT). Anasisitiza pia umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika kukuza usawa wa kijinsia, kama ilivyoonyeshwa na utiaji saini wa Mkataba wa Makubaliano kati ya SUA na Chuo Kikuu cha Sayansi za Maisha cha Norway (NMBU).

Kwa kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa pamoja, tunaweza kuhamasisha umoja na ushirikiano katika kujenga jamii bora yenye usawa na maendeleo endelevu.

Na. Edson Kanisa

 

Related Posts